top of page

KATIKA UWEPO WA BWANA

KARIBU

KANISA LA KISWAHILI 
NCHINI MAREKANI NA KWINGINEKO

Kanisa la The Way Gospel Church limeitwa kuzifikia jumuia za watu wanaozungumza lugha ya Swahili ndani na nje ya Marekani. Yesu aliwaamuru wanafunzi wake ya kuwa "enendeni, mkawafanye mataifa wote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu,..." (Mathayo 28:19). Kuna mamilioni ya watu wanaozungumza lugha ya Kiswahili ndani ya nchi ya Marekani ambao hawapati vizuri huduma ya neno la Mungu. Kuna mamilioni pia ambao wanaelewa kiingereza na lugha zingine za kimataifa lakini wangebarikiwa zaidi wakimwabudu Mungu katika lugha na mahadhi ya utamaduni wao. Kanisa la The Way Gospel Church lipo hapa kutimiza wito wa kitume wakati likichagiza lugha ya Kiswahili pia ambayo inawaunganisha mamilioni ya watu ndani na nje ya nchi ya Marekani. 

Image by Edward Cisneros
KUHUSU SISI

Huduma ya The Way Gospel Church imejengwa katika msingi wa Yesu Kristo, Maandiko Matakatifu kama yalivyoandikwa na kuvuviwa katika Biblia Takatifu, na uongozi wa Roho Mtakatifu. 

Image by James Coleman
HUDUMA

Huduma zetu zinalenga kumhubiri Kristo, na kugusa mahitaji ya jamii, hususani ya watu wanaoongea lugha ya Kiswahili.

Image by Aaron Burden
NENO LA LEO 

'Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. '

2 Wakorintho 12:9 

MAOMBI ya kila siku
IBADA YA JUMAPILI
MAOMBI MAALUM

J'tatu-Ijumaa: Maombi ya Pamoja 

Asubuhi 5:00AM-6:00AM

Mchana 1:00PM-2:00PM

Jioni 9:00PM-10:00PM

Jumamos: Maombi ya Wanawake

Jioni 9:00PM-10:00PM

Namna ya Kushiriki

Piga namba: +1 857 347 0566

(utaunganishwa moja kwa moja)

Maombi: 1:30PM-2:00PM 

Ibada ya Jumapili: 2:00PM-4:00PM

 

NJOO, TUMWABUDU MUNGU KWA UMOJA!

 

Namna ya kushiriki kwa njia ya mtandao

Piga namba: +1 857 347 0566

(utaunganishwa moja kwa moja)

Ijumaa: Maombezi 

Jioni 10:00PM-11:00PM

kiwa unahitaji kuhudumiwa na watumishi wa Mungu, andika ujumbe wa WhatsApp kwenye namba ya Kanisa ifuatayo, na utaunganishwa na watumishi wa Mungu wakati wowote.

+1 202 913 8912

(The Way Gospel Church)

NJOO. TUFANYE MABADILIKO. PAMOJA.

Unaweza kubadilisha maisha ya mtu kwa kitu kidogo kama kikombe cha kahawa.

bottom of page